وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذۡ يَتَوَفَّى ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ يَضۡرِبُونَ وُجُوهَهُمۡ وَأَدۡبَٰرَهُمۡ وَذُوقُواْ عَذَابَ ٱلۡحَرِيقِ
Na laiti ungeli ona Malaika wanapo wafisha wale walio kufuru wakiwapiga nyuso zao na migongo yao, na kuwaambia: Ionjeni adhabu ya Moto!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau ingalionekana, ewe Mtume, hali ya Malaika ya kuzichukua roho za Makafiri na kuzitoa, na huku wao wanawapiga nyuso zao wakiwaelekea, na wanawapiga migongo yao wakiwakimbia na wanawaambia, «Onjeni adhabu inayounguza», ungaliona jambo kubwa. Na msururu huu wa maneno ingawa sababu yake ni vita vya Badr, lakini unakusanya hali ya kila kafiri.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس