إِنَّ شَرَّ ٱلدَّوَآبِّ عِندَ ٱللَّهِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ
Hakika vinyama vilio viovu kabisa mbele ya Mwenyezi Mungu ni wale wanao kufuru, basi hao hawaamini;
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wabaya mno wa wale wanaotembea juu ya ardhi mbele ya Mwenyezi Mungu ni Makafiri wanaoendeleza ukafiri; wao hawawaamini Mitume wa Mwenyezi Mungu, hawaukubali upweke Wake wala hawazifuati sheria Zake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس