ٱلَّذِينَ عَٰهَدتَّ مِنۡهُمۡ ثُمَّ يَنقُضُونَ عَهۡدَهُمۡ فِي كُلِّ مَرَّةٖ وَهُمۡ لَا يَتَّقُونَ
Wale ambao miongoni mwao umepatana nao ahadi, kisha wanavunja ahadi yao kila mara, wala hawamchi Mungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Miongoni mwa wabaya hao ni Mayahudi ambao waliingia pamoja na wewe katika mapatano kwamba hawatakupiga vita wala hawatamsaidia yoyote dhidi yako, kisha wanazivunja ahadi zao mara kwa mara hali ya kuwa wao hawamuogopi Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس