ثُمَّ يَتُوبُ ٱللَّهُ مِنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَ عَلَىٰ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Kisha baada ya hayo Mwenyezi Mungu atawasamehe awatakao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na atakayerudi nyuma akaacha ukafiri wake baada ya hilo, na akaingia kwenye Uislamu, basi Mwenyezi Mungu Anaikubali toba ya Anayemtaka katika wao na Anamsamehe dhambi zake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, ni mwingi wa kurehemu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس