لَا يَسۡتَـٔۡذِنُكَ ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ أَن يُجَٰهِدُواْ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡۗ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلۡمُتَّقِينَ
Hawatakuomba ruhusa wale wanao muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, wasende kupigana Jihadi kwa mali yao na nafsi zao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwajua wachamngu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Si katika misimamo ya wanaomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na Siku ya Mwisho kukutaka ruhusa, ewe Nubii, ya kusalia nyuma kwa kutoshiriki kwenye jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa nafsi na mali. Hiyo ni misimamo ya wanafiki tu. Na Mwenyezi Mungu Anamjua Anayemuogopa Yeye na kumcha kwa kuzitekeleza faradhi Zake na kujitenga na Makatazo Yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس