أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Mwenyezi Mungu amewatengenezea Bustani zipitazo mito kati yake, wadumu humo. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Amewatayarishia Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama, mabustani ya Pepo ambayo inapita mito chini ya miti yake, hali ya kukaa humo milele. Huko ndiko kufaulu kukubwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس