قُلۡ سِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَٱنظُرُواْ كَيۡفَ بَدَأَ ٱلۡخَلۡقَۚ ثُمَّ ٱللَّهُ يُنشِئُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأٓخِرَةَۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Sema: Tembeeni katika ardhi na tazameni jinsi alivyo anzisha uumbaji; kisha Mwenyezi Mungu ndiye anaye umba umbo la baadaye. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza juu ya kila kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sema, ewe Mtume, kuwaambia wenye kukanusha kufufuliwa baada ya kufa, «Endeni katika ardhi, muangalie namna Mwenyezi Mungu Alivyoanzisha uumbaji na Asielemewe kuuanzisha hapo mwanzo?» Hivyo basi Hataelemewa na kule kuuanzilisha upya uanzilishaji mwingine. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu, hakuna jambo lolote Alitakalo linalomshinda.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس