وَمَآ أَنتُم بِمُعۡجِزِينَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا فِي ٱلسَّمَآءِۖ وَمَا لَكُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ مِن وَلِيّٖ وَلَا نَصِيرٖ
Na nyinyi si wenye kushinda katika ardhi wala katika mbingu. Wala nyinyi hamna mlinzi wala msaidizi isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hamkuwa nyinyi, enyi watu, ni wenye kumshinda Mwenyezi Mungu katika ardhi wala katika mbingu iwapo mtamuasi. Na nyinyi hamuna badala ya Mwenyezi Mungu mtegemewa yoyote wa kuyasimamia mambo yenu, wala msaidizi wa kuwaokoa nyinyi na Mwenyezi Mungu iwapo Anawatakia mabaya.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس