إِذۡ جَآءُوكُم مِّن فَوۡقِكُمۡ وَمِنۡ أَسۡفَلَ مِنكُمۡ وَإِذۡ زَاغَتِ ٱلۡأَبۡصَٰرُ وَبَلَغَتِ ٱلۡقُلُوبُ ٱلۡحَنَاجِرَ وَتَظُنُّونَ بِٱللَّهِ ٱلظُّنُونَا۠
Walipo kujieni kutoka juu yenu, na kutoka chini yenu; na macho yalipo kodoka, na nyoyo zikapanda kooni, nanyi mkamdhania Mwenyezi Mungu dhana mbali mbali.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kumbukeni pindi walipowajia kwa juu yenu kutoka sehemu ya juu ya bonde lilioko upande wa mashariki na kwa chini yenu kutoka sehemu ya kati ya bonde lilioko upande wa magharibi, na pindi macho yalipokodoka kwa kuduwaa sana na kushutuka, na nyoyo zikafika kwenye magorombo (ya koo) kwa kitisho kikali, na wanafiki wakajawa na ukataji tamaa na uvumi ukazidi, na mkawa mnamdhania Mwenyezi Mungu dhana mbaya ya kuwa Yeye Hataiokoa Dini Yake na Hatalikuza jina Lake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس