لِيُكَفِّرَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ أَسۡوَأَ ٱلَّذِي عَمِلُواْ وَيَجۡزِيَهُمۡ أَجۡرَهُم بِأَحۡسَنِ ٱلَّذِي كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Ili Mwenyezi Mungu awafutie ukomo wa uovu walio ufanya na awalipe ujira wao kwa mujibu wa ukomo wa wema walio kuwa wakiutenda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ili Mwenyezi Mungu Awafutie yale maovu zaidi ya matendo waliyoyafanya ulimwenguni kwa sababu ya kile walichokifanya cha kurudi kwa Mwenyezi Mungu kwa kutubia makosa waliyoyatenda huko, na ili Mwenyezi Mungu Awalipe mema, kwa utiifu wao ulimwenguni, malipo mazuri zaidi ya matendo ambayo walikuwa wakiyafanya, nayo ni Pepo,
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس