فَإِذَا مَسَّ ٱلۡإِنسَٰنَ ضُرّٞ دَعَانَا ثُمَّ إِذَا خَوَّلۡنَٰهُ نِعۡمَةٗ مِّنَّا قَالَ إِنَّمَآ أُوتِيتُهُۥ عَلَىٰ عِلۡمِۭۚ بَلۡ هِيَ فِتۡنَةٞ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Na dhara inapo mgusa mtu hutuomba. Kisha tunapo mpa neema zitokazo kwetu, husema: Nimepewa haya kwa sababu ya ilimu yangu. Sio! Huo ni mtihani! Lakini wengi wao hawajui!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na ikimpata mwanadamu shida na madhara humuomba Mola wake amuondolee, na tunapomuondolea yaliyompata na tukampa neema kutoka kwetu hurudi kumkanusha Mola wake na kukataa wema Wake na huwa akisema, «Haya niliyopewa yatokamana na ujuzi wa Mwenyezi Mungu kuwa mimi ninafaa na ninastahiki kuyapata. Bali huo ni mtihani wa Mwenyezi Mungu kuwatahini waja Wake, ili Atazame ni yupi anayemshukuru kwa kumtenga na anayemkanusha. Lakini wengi wao, kwa ujinga wao na dhana zao mbaya, hawajui kuwa hayo ni mavuto kideogo-kidogo kutoka kwa Mwenyezi Mungu na ni mtihani kwao kuhusu kushukuru neema.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس