إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَهَٰمَٰنَ وَقَٰرُونَ فَقَالُواْ سَٰحِرٞ كَذَّابٞ
Kumwendea Firauni na Hamana na Qaruni, wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo mkubwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Apate kuenda kwa Fir'awn, mfalme wa Misri, na Hāmān waziri wake, na Qārūn mwenye mali mengi na mahazina ya vitu vya thamani, wakaukanusha utume wake na wakafanya kiburi na wakamwambia, «Yeye ni mchawi mrongo sana, basi ni vipi anadai kuwa yeye ametumilizwa kwa watu kuwa ni Mtume?»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس