لَّا يَسۡـَٔمُ ٱلۡإِنسَٰنُ مِن دُعَآءِ ٱلۡخَيۡرِ وَإِن مَّسَّهُ ٱلشَّرُّ فَيَـُٔوسٞ قَنُوطٞ
Mwanaadamu hachoki kuomba dua za kheri, na inapo mpata shari, mara huvunjika moyo akakata tamaa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Binadamu hachoki kumuomba Mola wake Ampatie mema ya duniani, na akipatikana na umasikini na shida, huwa anakata tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu na anakufa moyo kwa kuwa na dhana mbaya kwa Mola wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس