إِذۡ يُوحِي رَبُّكَ إِلَى ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ أَنِّي مَعَكُمۡ فَثَبِّتُواْ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْۚ سَأُلۡقِي فِي قُلُوبِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ ٱلرُّعۡبَ فَٱضۡرِبُواْ فَوۡقَ ٱلۡأَعۡنَاقِ وَٱضۡرِبُواْ مِنۡهُمۡ كُلَّ بَنَانٖ
Mola wako Mlezi alipo wafunulia Malaika: Hakika Mimi ni pamoja nanyi, basi watieni nguvu walio amini. Nitatia woga katika nyoyo za walio kufuru. Basi wapigeni juu ya shingo na wapigeni kwenye kila ncha za vidole.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Pindi Mola wako, ewe Nabii, Alipowapelekea wahyi Malaika ambao Mwenyezi Mungu Aliwasaidia nao Waislamu katika vita vya Badr, «Mimi nipo na nyinyi, nawasaidia na kuwahami, watieni hima wale walioamini, nitaweka kwenye nyoyo za waliokanusha kicho kingi, unyonge na utwevu.» Vipigeni, enyi Waumini, vichwa vya makafiri na wapigeni wao kila ncha na kila kiungo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس