ذَٰلِكُمۡ وَأَنَّ ٱللَّهَ مُوهِنُ كَيۡدِ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Ndio hivyo! Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kudhoofisha vitimbi vya makafiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kitendo hiki cha kuwaua washirikina na kuwarushia waliposhindwa na mtihani mzuri wa kuwapa ushindi Waumini juu ya maadui zao, huo unatoka kwa Mwenyezi Mungu kuja kwa Waumini, na kwamba Mwenyezi Mungu, mbeleni, ni mwenye kuvikosesha nguvu na kuvimaliza vitimbi vya makafiri mpaka wawe wanyonge na wafuate haki au waangamie.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس