وَقَٰتِلُوهُمۡ حَتَّىٰ لَا تَكُونَ فِتۡنَةٞ وَيَكُونَ ٱلدِّينُ كُلُّهُۥ لِلَّهِۚ فَإِنِ ٱنتَهَوۡاْ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِمَا يَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ
Na piganeni nao mpaka isiwepo fitna na mateso, na Dini yote iwe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Lakini wakiacha, basi hakika Mwenyezi Mungu anayaona wanayo yatenda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na piganeni na washirikina, enyi waumini, mpaka usiweko ushirikina na uzuiliaji wa njia ya Mwenyezi Mungu na kusiabudiwe isipokuwa Mwenyezi Mungu Peke Yake Asiye na mshirika, ili chuki ziwaondokee waja wa Mwenyezi Mungu katika ardhi na mpaka dini, utiifu na ibada vitakasiwe Mwenyezi Mungu tu bila mwingine. Wakiwa watakomeka na kuwafitini Waumini na kumshirikisha Mwenyezi Mungu na wakawa kwenye dini ya haki pamoja na nyinyi, basi Mwenyezi Mungu hakifichiki Kwake wanachokifanya cha kuacha ukafiri na kuingia kwenye Uislamu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس