لَّوۡلَا كِتَٰبٞ مِّنَ ٱللَّهِ سَبَقَ لَمَسَّكُمۡ فِيمَآ أَخَذۡتُمۡ عَذَابٌ عَظِيمٞ
Lau isingeli kuwa hukumu iliyo kwisha tangulia kutoka kwa Mwenyezi Mungu ingeli kupateni adhabu kubwa kwa vile mlivyo chukua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Lau si Kitabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu chenye mapitisho na Makadirio yaliyotangulia ya kuhalalisha ngawira na kukomboa mateka kwa umma huu, basi ingaliwapata adhabu kubwa kwa kuchukuwa kwenu ngawira na fidia kabla ya kuletwa sheria kuhusu mambo mawili hayo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس