لَا يَرۡقُبُونَ فِي مُؤۡمِنٍ إِلّٗا وَلَا ذِمَّةٗۚ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُعۡتَدُونَ
Hawatazami kwa Muumini udugu wala ahadi; basi hao ndio warukao mipaka.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Washirikina hawa wako kwenye vita dhidi ya Imani na watu wake, hawauekei uzito wowote ujamaa wa Muumini wala mapatano yake; walilonalo wao ni uadui na udhalimu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس