يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ قَٰتِلُواْ ٱلَّذِينَ يَلُونَكُم مِّنَ ٱلۡكُفَّارِ وَلۡيَجِدُواْ فِيكُمۡ غِلۡظَةٗۚ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ مَعَ ٱلۡمُتَّقِينَ
Enyi mlio amini! Piganeni na wale makafiri walio karibu yenu, na wakute ugumu kwenu. Na jueni ya kwamba Mwenyezi Mungu yu pamoja na wacha- Mngu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi ambao mlimuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkaifuata sheria Yake kivitendo, anzeni kupigana na walio karibukaribu na Nyumba ya Uislamu , miongoni mwa makafiri, na wakute kutoka kwenu ushupavu na ukali. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wachamungu kwa msaada Wake na nusura Yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس