فَلَا تُعۡجِبۡكَ أَمۡوَٰلُهُمۡ وَلَآ أَوۡلَٰدُهُمۡۚ إِنَّمَا يُرِيدُ ٱللَّهُ لِيُعَذِّبَهُم بِهَا فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَتَزۡهَقَ أَنفُسُهُمۡ وَهُمۡ كَٰفِرُونَ
Yasikufurahishe mali yao wala wana wao. Hakika Mwenyezi Mungu anataka kuwaadhibu kwayo hapa duniani, na zitoke roho zao na hali wao ni makafiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Zisikushangaze, ewe Nabii, mali za wanafiki hawa wala watoto wao. Hakika Mwenyezi Mungu Anataka kuwaadhibu kwa hizo hapa ulimwenguni, kwa tabu ya kuzipata na kwa mikasa inayozifikia kwa kuwa yatokeyapo hayo hawatarajii malipo mema kwa Mwenyezi Mungu, na zitoke nafsi zao wapate kufa juu ya kumkanusha Mwenyezi Mungu na Mtume Wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس