لَٰكِنِ ٱلرَّسُولُ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَعَهُۥ جَٰهَدُواْ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡۚ وَأُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمُ ٱلۡخَيۡرَٰتُۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ
Lakini Mtume na wale walio amini pamoja naye waliwania Jihadi kwa mali zao na nafsi zao. Hao ndio watakao pata kheri nyingi, na hao ndio wenye kufanikiwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Iwapo wanafiki hawa watajikalisha nyuma waache kupigana, Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, amepigana jihadi, yeye na Waumini pamoja naye, kwa mali zao na nafsi zao. Wao wamepata ushindi na ngawira ulimwenguni, na watapata Pepo na mapokezi mema kesho Akhera. Na wao ndio wenye kufaulu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس