وَلَا عَلَى ٱلَّذِينَ إِذَا مَآ أَتَوۡكَ لِتَحۡمِلَهُمۡ قُلۡتَ لَآ أَجِدُ مَآ أَحۡمِلُكُمۡ عَلَيۡهِ تَوَلَّواْ وَّأَعۡيُنُهُمۡ تَفِيضُ مِنَ ٱلدَّمۡعِ حَزَنًا أَلَّا يَجِدُواْ مَا يُنفِقُونَ
Wala wale walio kujia ili uwachukue ukasema: Sina kipando cha kukuchukueni. Tena wakarudi na macho yao yanamiminika machozi kwa huzuni ya kukosa cha kutoa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Pia hapana makosa kwa wale ambao wakikujia kutaka uwasaidie kuwachukua kwenda kwenye jihadi, unawaambia, «Sina wanyama wa mimi kuwapatia muwapande», hapo wakakuacha na kugeuka kwenda zao, na macho yao yanabubujika machozi kwa masikitiko ya kukosa utukufu wa jihadi na thawabu zake kwa kuwa hawakupata cha kutumia na cha kuwabeba lau walitoka kwenda kupigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس