يُعَذِّبُ مَن يَشَآءُ وَيَرۡحَمُ مَن يَشَآءُۖ وَإِلَيۡهِ تُقۡلَبُونَ
Humuadhibu amtakaye, na humrehemu amtakaye. Na kwake Yeye mtapelekwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Anamuadhibu Anayemtaka kati ya viumbe Vyake kwa makosa waliyoyafanya siku za uhai wao, na Anawarehemu Anaowataka miongoni mwao, kati ya wale waliotubia, wakaamini na wakafanya matendo mema. Na Kwake Yeye mtarejeshwa muhesabiwe na mulipwe kwa mliyoyafanya.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس