وَقَالُواْ لَوۡلَآ أُنزِلَ عَلَيۡهِ ءَايَٰتٞ مِّن رَّبِّهِۦۚ قُلۡ إِنَّمَا ٱلۡأٓيَٰتُ عِندَ ٱللَّهِ وَإِنَّمَآ أَنَا۠ نَذِيرٞ مُّبِينٌ
Na walisema: Mbona hakuteremshiwa Ishara kutoka kwa Mola wake Mlezi? Sema: Ishara ziko kwake Mwenyezi Mungu; ama mimi kwa hakika ni mwonyaji mwenye kubainisha tu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na washirikina walisema, «Si ateremshiwe Muammad dalili na hoja kutoka kwa Mola wake, kama vile ngamia wa Ṣāliḥ na fimbo ya Mūsā!» Waambie, «Jambo la miujiza hii liko kwa Mwenyezi Mungu, Akitaka Ataiteremsha na Akitaka Ataizuia. Na hakika ni kwamba mimi ni muonyaji, ninawatahadharisha na ukali wa adhabu Yake na mateso Yake, na ni mwenye kuwaonyesha njia ya haki na batili.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس