أَوَلَمۡ يَكۡفِهِمۡ أَنَّآ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ يُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَرَحۡمَةٗ وَذِكۡرَىٰ لِقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ
Je! Kwani hayakuwatosha ya kwamba tumekuteremshia Kitabu hiki wanacho somewa? Hakika katika hayo zipo rehema na mawaidha kwa watu wanao amini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kwani haikuwatosha washirikina hawa ili wajue ukweli wako, ewe Mtume, kuwa sisi tumekuteremshia Qur’ani inayosomwa kwao? Hakika katika hii Qur’ani kuna rehema kwa Waumini, ulimwenguni na Akhera, na kuna ukumbusho wa kujikumbusha nao wa mazingatio na mawaidha.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس