هُنَالِكَ ٱبۡتُلِيَ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَزُلۡزِلُواْ زِلۡزَالٗا شَدِيدٗا
Hapo ndipo Waumini walipo jaribiwa, na wakatikiswa mtikiso mkali.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Katika msimamo huo mgumu, Imani za Waumini zilijaribiwa na watu wakakaguliwa, na akajulikana mnafiki kwa kutengwa na Muumini, na wakasukikasukika msukosuko mkali kwa kuingiwa na kicho na babaiko, ili Imani yao ibainike na yakini yao izidi
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس