إِنَّ ٱلَّذِينَ يُؤۡذُونَ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ لَعَنَهُمُ ٱللَّهُ فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِ وَأَعَدَّ لَهُمۡ عَذَابٗا مُّهِينٗا
Hakika wanao muudhi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, Mwenyezi Mungu amewalaani duniani na Akhera, na amewaandalia adhabu ya kufedhehi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika ya wale wanaomuudhi Mwenyezi Mungu kwa kumshirikisha na kufanya maasia mengine, na wakamuudhi Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa maneno na vitendo, Mwenyezi Mungu atawafukuza na Atawaweka mbali na kheri duniani na Akhera, na Amewaandalia, huko Akhera, adhabu kali yenye kuwadhalilisha na kuwafanya wanyonge.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس