وَلَوۡ أَنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ مَا فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا وَمِثۡلَهُۥ مَعَهُۥ لَٱفۡتَدَوۡاْ بِهِۦ مِن سُوٓءِ ٱلۡعَذَابِ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ وَبَدَا لَهُم مِّنَ ٱللَّهِ مَا لَمۡ يَكُونُواْ يَحۡتَسِبُونَ
Na lau kuwa walio dhulumu wangeli kuwa na vyote viliomo duniani na pamoja navyo vingine kama hivyo, bila ya shaka wangeli vitoa kujikomboa katika adhabu mbaya hiyo Siku ya Kiyama. Na yatawadhihirikia kwa Mwenyezi Mungu wasiyo kuwa wakiyatarajia.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau hao wanaomshirikisha Mwenyezi Mungu wangalikuwa nacho kila kilichoko kwenye ardhi miongoni mwa mali, vitu vya thamani na vingine mfano wake pamoja navyo kuongezea, wangalikitoa Siku ya Kiyama ili wajikomboe kwacho na adhabu mbaya. Na lau wangalikitoa na wakataka kujikomboa kwacho hakingalikubaliwa kutoka kwao na hakingaliwafalia kitu chochote kuwaepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu. Na itawadhihirikia wao Siku hiyo amri ya Mwenyezi Mungu na adhabu Yake wasizokuwa wakizidhania duniani kuwa zitawashukia.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس