أَلَآ إِنَّهُمۡ فِي مِرۡيَةٖ مِّن لِّقَآءِ رَبِّهِمۡۗ أَلَآ إِنَّهُۥ بِكُلِّ شَيۡءٖ مُّحِيطُۢ
Ama wao wamo katika shaka ya kukutana na Mola wao Mlezi! Ama hakika Yeye amekizunguka kila kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Jueni na mtanabahi kuwa hawa makafiri wako kwenye shaka kubwa kuhusu kufufuliwa baada ya kufa. Jueni na mtanabahi kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, Amekizunguka kila kitu kwa ujuzi, uweza na ushindi, hakuna chochote kinachofichamana Kwake ardhini wala mbinguni.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس