فَكَأَيِّن مِّن قَرۡيَةٍ أَهۡلَكۡنَٰهَا وَهِيَ ظَالِمَةٞ فَهِيَ خَاوِيَةٌ عَلَىٰ عُرُوشِهَا وَبِئۡرٖ مُّعَطَّلَةٖ وَقَصۡرٖ مَّشِيدٍ
Miji mingapi tuliiangamiza iliyo kuwa ikidhulumu, ikawa imebaki magofu, na visima vilivyo achwa, na majumba yaliyo kuwa madhubuti?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ni miji mingi iliyojidhulumu kwa ukafiri wake, tuliwaangamiza watu wake, nyumba zao zikavunjwa zikawa ziko tupu hazina wakazi wake, visima vyake vikawa havichotwi maji na majumba yake ya fahari yaliyo marefu yaliyopambwa hayakuwakinga watu wake na adhabu kali.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس