وَمَا كُنتَ تَتۡلُواْ مِن قَبۡلِهِۦ مِن كِتَٰبٖ وَلَا تَخُطُّهُۥ بِيَمِينِكَۖ إِذٗا لَّٱرۡتَابَ ٱلۡمُبۡطِلُونَ
Na wewe hukuwa kabla yake unasoma kitabu chochote, wala hukukiandika kwa mkono wako wa kulia. Ingeli kuwa hivyo wangeli fanya shaka wavunjifu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na miongoni mwa miujiza yako iliyo wazi, ewe Mtume, ni kuwa wewe hukusoma kitabu wala hukuandika herufi zozote kwa mkono wako wa kulia kabla ya hii Qur’ani kukuteremkia, na hali wao wanalijua hilo. Na lau ungalikuwa ni mwenye kusoma au kuandika kabla hujaletewa wahyi wangalilifanyia shaka hilo hao wapotofu na wangalisema, «Amejifunza hiyo (Qur’ani) au ameinakili kutoka kwenye vitabu vilivyotangulia.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس