ٱللَّهُ يَبۡسُطُ ٱلرِّزۡقَ لِمَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦ وَيَقۡدِرُ لَهُۥٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ
Mwenyezi Mungu humkunjulia, na humdhikishia, riziki amtakaye katika waja wake. Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu, aliyetakasika na kuwa juu, Anampanulia riziki Anayemtaka na Anawabania wengine katika wao, kwa kuwa Anayajua yanayowafaa waja Wake. Hakika Mwenyezi Mungu kwa kila jambo, katika hali zenu na mambo yenu, ni Mjuzi, hakuna chochote kinachofichamana Kwake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس