إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَظَلَمُواْ لَمۡ يَكُنِ ٱللَّهُ لِيَغۡفِرَ لَهُمۡ وَلَا لِيَهۡدِيَهُمۡ طَرِيقًا
Hakika wale walio kufuru na wakadhulumu hawi Mwenyezi Mungu kuwasamehe wala kuwaongoa njia.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wale waliomkanusha Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakadhulumu kwa kuendelea kwao na ukafiri, Mwenyezi Mungu Hatakuwa ni Mwenye kuwasamehe madhambi yao wala kuwaongoza njia ya kuwaokoa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس