فَكَيۡفَ إِذَا جِئۡنَا مِن كُلِّ أُمَّةِۭ بِشَهِيدٖ وَجِئۡنَا بِكَ عَلَىٰ هَـٰٓؤُلَآءِ شَهِيدٗا
Basi itakuwaje pindi tukiwaletea kutoka kila umma shahidi, na tukakuleta wewe kuwa shahidi wa hawa?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Vipi itakuwa hali ya watu, Siku ya Kiyama, pindi Mwenyezi Mungu Atakapomleta Mtume wa kila uma, ili atoe ushahidi juu yake kwa yale uliyoyafanya, na atakapo kukuleta wewe, ewe Mtume, utoe ushahidi juu ya uma wako kwamba wewe uliwafikishia ujumbe wa Mola wako?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس