فَقَٰتِلۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ لَا تُكَلَّفُ إِلَّا نَفۡسَكَۚ وَحَرِّضِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۖ عَسَى ٱللَّهُ أَن يَكُفَّ بَأۡسَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ وَٱللَّهُ أَشَدُّ بَأۡسٗا وَأَشَدُّ تَنكِيلٗا
Basi pigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu. Hukalifishwi ila nafsi yako tu. Na wahimize Waumini. Huenda Mwenyezi Mungu akayazuia mashambulio ya walio kufuru. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mkali zaidi wa kushambulia na Mkali zaidi wa kuadhibu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Basi pigana jihadi, ewe Nabii, katika njia ya Mwenyezi Mungu na kulitukuza neno Lake. Hulazimishwi kitendo cha asiyekuwa wewe wala hutaadhibiwa kwacho. Na wahimize Waumini kupigana jihadi na uwavutie wafanye hivyo, kwani huenda Mwenyezi Mungu Akazuia, kwa ajili yako na wao, mashambulizi ya makafiri na nguvu zao. Na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Ana nguvu nyingi zaidi na Ana adhabu kubwa zaidi kwa makafiri.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس