۞فَمَا لَكُمۡ فِي ٱلۡمُنَٰفِقِينَ فِئَتَيۡنِ وَٱللَّهُ أَرۡكَسَهُم بِمَا كَسَبُوٓاْۚ أَتُرِيدُونَ أَن تَهۡدُواْ مَنۡ أَضَلَّ ٱللَّهُۖ وَمَن يُضۡلِلِ ٱللَّهُ فَلَن تَجِدَ لَهُۥ سَبِيلٗا
Mmekuwaje kuwa makundi mawili kwa khabari ya wanaafiki, na hali Mwenyezi Mungu amewageuza kwa sababu ya yale waliyo yachuma? Je! Mnataka kumwona mwongofu ambaye Mwenyezi Mungu amemhukumu kuwa kapotea? Na aliye mhukumu Mwenyezi Mungu kuwa amekwisha potea wewe hutampatia njia.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Muna nini nyinyi, enyi Waumini, mumetafautiana makundi mawili kuhusu wanafiki: kundi linasema kwamba wapigwe vita na lingine halisemi hivyo? Na hali Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Amewatia kwenye ukafiri na upotevu kwa sababu ya vitendo vyao. Kwani mnataka kumpa uongofu yule ambaye Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Ameuepusha moyo wake na dini Yake? Na yoyote ambaye Mwenyezi Mungu Ameacha kumuafikia kufuata dini Yake na yale Aliyoyaamrisha, basi hana njia ya kufikia kwenye uongofu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس