أَلَمۡ يَأۡتِهِمۡ نَبَأُ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ قَوۡمِ نُوحٖ وَعَادٖ وَثَمُودَ وَقَوۡمِ إِبۡرَٰهِيمَ وَأَصۡحَٰبِ مَدۡيَنَ وَٱلۡمُؤۡتَفِكَٰتِۚ أَتَتۡهُمۡ رُسُلُهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِۖ فَمَا كَانَ ٱللَّهُ لِيَظۡلِمَهُمۡ وَلَٰكِن كَانُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ
Je, hazikuwafikia khabari za walio kuwa kabla yao - kaumu ya Nuhu, na A'ad, na Thamud, na kaumu ya Ibrahim, na watu wa Madyana, na miji iliyo pinduliwa chini juu? Mitume wao waliwafikia kwa hoja zilizo wazi. Basi Mwenyezi Mungu hakuwa mwenye kuwadhulumu, walakini wao walikuwa wakijidhulumu wenyewe.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kwani haikuwajia wanafiki hawa habari ya wale waliopita, miongoni mwa watu wa Nūḥ, kabila la 'Ād, kabila la Thamūd, watu wa Ibrāhīm, watu wa Madyan na watu wa Lūṭ, walipowajia Mitume na wahyi na aya za Mwenyezi Mungu wakawakanusha? Wote hawa Mwenyezi Mungu Aliwateremshia adhabu Yake, kuwalipiza wao kwa matendo yao mabaya. Mwenyezi Mungu Hakuwa ni mwenye kuwadhulumu, lakini ni wao wenyewe walijidhulumu nafsi zao kwa kukanusha na kupinga.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس