إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ يَهۡدِيهِمۡ رَبُّهُم بِإِيمَٰنِهِمۡۖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهِمُ ٱلۡأَنۡهَٰرُ فِي جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Hakika walio amini na wakatenda mema, Mola wao Mlezi atawaongoa kwa sababu ya Imani yao. Itakuwa inapita mito kati yao katika Mabustani yenye neema.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika ya wale ambao walimuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya mema, Mola wao Atawaonesha njia ya Pepo na Atawaafikia kufanya matendo yenye kuwafikisha kwake, kwa sababu ya Imani yao , kisha Atawapa malipo mema kwa kuingia Peponi na kuwashushia wao radhi Zake; chini ya sebule zao na majumba yao itakuwa ikipita mito, wakiwa ndani ya mabustani ya Pepo ya starehe.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس