وَلَقَدۡ صَرَّفۡنَا فِي هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانِ لِلنَّاسِ مِن كُلِّ مَثَلٖۚ وَكَانَ ٱلۡإِنسَٰنُ أَكۡثَرَ شَيۡءٖ جَدَلٗا
Na bila ya shaka tumewaelezea watu katika hii Qur'ani kila namna ya mfano. Lakini mwanaadamu amezidi kuliko kila kitu kwa ubishi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kwa hakika tumeeleza na kufafanua katika hii Qur’ani aina nyingi ya mifano ili waaidhike na waamini. Na mwanadamu ni mwingi wa utesi na ubishi miongoni mwa viumbe.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس