وَمِنَ ٱلنَّاسِ مَن يُجَٰدِلُ فِي ٱللَّهِ بِغَيۡرِ عِلۡمٖ وَيَتَّبِعُ كُلَّ شَيۡطَٰنٖ مَّرِيدٖ
Na miongoni mwa watu wapo wanao bishana juu ya Mwenyezi Mungu bila ya ilimu, na wanamfuata kila shet'ani aliye asi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na baadhi ya vichwa vya ukafiri miongoni mwa watu wanaleta utesi na wanatilia shaka uweza wa Mwenyezi Mungu wa kufufua, kwa ujinga wao wa kutojua uhakika wa uweza huu na kwa kumfuata kila shetani mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mitume Wake kati ya viongozi wa upotevu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس