لِّيَجۡعَلَ مَا يُلۡقِي ٱلشَّيۡطَٰنُ فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡقَاسِيَةِ قُلُوبُهُمۡۗ وَإِنَّ ٱلظَّـٰلِمِينَ لَفِي شِقَاقِۭ بَعِيدٖ
Hayo ni ili alifanye lile analo litia Shet'ani liwe ni fitna kwa wale wenye maradhi ndani ya nyoyo zao, na wale ambao nyoyo zao ni ngumu. Na hakika madhaalimu wamo katika mfarakano wa mbali.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hakikua kitendo hiki kutoka kwa Shetani isipokuwa Mwenyezi Mungu Akifanye ni mtihani kwa wale ambao ndani ya nyoyo zao muna shaka na unafiki na kwa wale washirikina washupavu wa nyoyo ambao haliathiri kwao kemeo lolote. Na kwa hakika, madhalimu miongoni mwa hawa na wale wako kwenye uadui mkubwa na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na upingaji haki ulio mbali na usawa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس