وَلَا يَزَالُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي مِرۡيَةٖ مِّنۡهُ حَتَّىٰ تَأۡتِيَهُمُ ٱلسَّاعَةُ بَغۡتَةً أَوۡ يَأۡتِيَهُمۡ عَذَابُ يَوۡمٍ عَقِيمٍ
Na walio kufuru hawatoacha kuwa katika wasiwasi kwa hilo mpaka Saa iwafikie ghafla, au iwafikie adhabu ya Siku Tasa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hawataacha makafiri wenye kukanusha kuendelea kuwa kwenye shaka juu ya Qur’ani uliokuja nayo mpaka Kiyama kiwajie kwa ghafula na hali wao wako juu ya ukanushaji wao, au iwajie wao adhabu ya Siku isiyokuwa na wema ndani yake, nayo ni Siku ya kiyama.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس