ٱلَّذِينَ يَتَّخِذُونَ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَوۡلِيَآءَ مِن دُونِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۚ أَيَبۡتَغُونَ عِندَهُمُ ٱلۡعِزَّةَ فَإِنَّ ٱلۡعِزَّةَ لِلَّهِ جَمِيعٗا
Wale ambao huwafanya makafiri kuwa ndio marafiki badala ya Waumini. Je! Wanataka wapate kwao utukufu? Basi hakika utukufu wote ni wa Mwenyezi Mungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ambao wanawategemea makafiri na kuwafanya ni wasaidizi wao, na wanaacha kuwapenda Waumini na kuwategemea, wala hawana haja ya mapenzi yao. Kwani wanatafuta, kwa hilo kuokolewa na kupata hifadhi kwa makafiri? Hili wao hawalimiliki. Kwani uokozi, enzi na nguvu, vyote ni vya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Peke Yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس