أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ لَعَنَهُمُ ٱللَّهُۖ وَمَن يَلۡعَنِ ٱللَّهُ فَلَن تَجِدَ لَهُۥ نَصِيرًا
Hao ndio Mwenyezi Mungu amewalaani. Na ambaye Mwenyezi Mungu amemlaani basi hutamwona kuwa na mwenye kumnusuru.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hao ndio ambao umezidi uharibifu wao na umeenea upotevu wao. Mwenyezi Mungu,Aliyetukuka, Amewatoa kwenye rehema Yake. Na yoyote ambaye Mwenyezi Mungu Anamfukuza kwenye rehema Yake, hutampatia wa kumnusuru na kumuepushia adhabu mbaya.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس