فَكُلُواْ مِمَّا ذُكِرَ ٱسۡمُ ٱللَّهِ عَلَيۡهِ إِن كُنتُم بِـَٔايَٰتِهِۦ مُؤۡمِنِينَ
Basi kuleni katika walio somewa jina la Mwenyezi Mungu, ikiwa mnaziamini Aya zake.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Basi kuleni, kati ya wanyama waliochinjwa, wale ambao jina la Mwenyezi Mungu lilitajwa wakati wa kuchinjwa, iwapo nyinyi mnaziamini hoja za Mwenyezi Mungu, aliyetukuka, zilizo wazi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس