ٱنظُرۡ كَيۡفَ كَذَبُواْ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِمۡۚ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ
Tazama jinsi wanavyo jisemea uwongo wenyewe. Na yamewapotea waliyo kuwa wakiyazua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Fikiri, ewe Mtume, vipi washirikina hawa wanasema urongo juu ya nafsi zao, na wao kesho Akhera watajiepusha na ushirikina! Yatawaondokea wao na kuwapotea yale waliokuwa wakiyadhania ya kuwa waungu wao watawaombea.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس