لِّكُلِّ نَبَإٖ مُّسۡتَقَرّٞۚ وَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَ
Kila khabari ina kipindi chake. Nanyi mtakuja jua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kila habari ina kituo cha kutulia na kikomo cha kukomea, hapo haki na batili zitafunuka. Na mtajua, enyi makafiri, mwisho wa jambo lenu, itakaposhuka adhabu ya Mwenyezi Mungu kwenu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس