وَلَا يَحۡسَبَنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ سَبَقُوٓاْۚ إِنَّهُمۡ لَا يُعۡجِزُونَ
Wala wasidhanie wale walio kufuru kwamba wao wametangulia mbele. La, wao hawatashinda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wasidhanie wale ambao walizikanusha aya za Mwenyezi Mungu kwamba wao washapita na washaokoka na kwamba Mwenyezi Mungu Hawawezi; hakika wao hawatakwepa adhabu ya Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس