فَهَلۡ يَنتَظِرُونَ إِلَّا مِثۡلَ أَيَّامِ ٱلَّذِينَ خَلَوۡاْ مِن قَبۡلِهِمۡۚ قُلۡ فَٱنتَظِرُوٓاْ إِنِّي مَعَكُم مِّنَ ٱلۡمُنتَظِرِينَ
Basi, je! Wanangojea jingine ila kama yaliyo tokea siku za watu walio pita kabla yao? Ngojeni! Nami ni pamoja nanyi katika wanao ngoja.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Je, hawa wanangojea isipokuwa hiyo siku watakapoishuhudia adhabu ya Mwenyezi Mungu mfano wa siku za wakale wao waliokanusha waliopita kabla yao? Sema, ewe Mtume, «Ingojeeni adhabu ya Mwenyezi Mungu; hakika mimi ni mwenye kuingojea pamoja na nyinyi kuteswa kwenu.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس