كَذَٰلِكَ حَقَّتۡ كَلِمَتُ رَبِّكَ عَلَى ٱلَّذِينَ فَسَقُوٓاْ أَنَّهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ
Ndio kama hivyo kauli ya Mola wako Mlezi itakavyo wathibitikia wale walio potoka, ya kwamba hawatoamini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kama walivyokanusha washirikina hawa na walivyoendelea kwenye ushirikina wao, ndivyo lilivothibiti neno la Mola wako, hukumu Yake na uamuzi Wake juu ya wale waliotoka nje ya utiifu Wake wakaenda kumuasi na wakamkanusha, kwamba wao hawataamini upweke wa Mwenyezi Mungu wala unabii wa Nabii Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amawni zimshukiye, wala hawatafanya matendo yanayolingana na uongofu Wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس